Baba yetu uliye mbinguni: Jina lako litukuzwe. Ufalme wako ufike. Utakalo lifanyike duniani kama mbinguni. Utupe leo chakula chetu tunachohitaji. Utusamehe makosa yetu, kama nasi tunavyowasamehe waliotukosea. Usitutie katika majaribu, lakini utuokoe na yule Mwovu. Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina. Mathayo Mtakatifu 6:9-13